Tayari wateja milioni mbili ambao hutumia huduma za benki wamejisajili kutumia huduma ya PesaLink, ambayo inamilikiwa na Chama cha Wamiliki wa Mabenki nchini (KBA). Huduma hiyo ilianzishwa miezi miwili iliyopita na kampuni ya kiteknolojia ya Integrated Payment Services Limited (IPSL), inayomilikiwa na KBA.
Jumla ya benki 22 ambazo zimeidhinishwa na Benki Kuu nchini (CBK) zinatumia huduma hiyo kuwezesha kuhamishwa kwa pesa kutoka kwa benki moja hadi nyingine.
PesaLink inapatikana kwa takriban benki tano na wateja wanaweza kuhamisha pesa kutoka benki moja hadi nyingine na kupokelewa papo hapo katika upande mwingine.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |