Ofisi ya kuratibu masuala ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan jana ilitoa ripoti ikisema katika miezi mitatu iliyopita ya mwaka huu, wakimbizi zaidi ya elfu 60 wa Sudan Kusini walikimbia vita na njaa kwenye maeneo ya magharibi na kusini ya nchi hiyo. Kabla ya hapo Shirika la Kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa lilikadiria kuwa wakimbizi elfu 60 wa Sudan Kusini wataingia nchini Sudan mwaka huu, lakini idadi hiyo imezidi katika miezi mitatu iliyopita.
Ripoti hiyo ilisema, hii inaonesha kuwa hali ya Sudan Kusini inazidi kuwa mbaya, na idadi ya wakimbizi inaweza kuongezeka hivi karibuni.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |