Mayweather kurejea rasmi ulingoni, kuzipiga na McGregor Juni 10 Las Vegas
(GMT+08:00) 2017-04-04 08:36:57
Wababe Floyd Mayweather na Conor McGregor watapigana Juni 10, mwaka huu. Mmarekani anayefahamika kama Money na Muireland aitwaye Notorious wameuteua ukumbi wa T-Mobile Arena mjini Las Vegas kuwa shehemu ya pambano lao.
Mayweather amesema kwamba rasmi amerejea ulingoni kwa ajili ya McGregor baada ya kustaafu akiwa amepigana mapambano 49 na kushinda yote.