Uvumi wa nyota huyo kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kwenda kujiunga na LA Galaxy ya Marekani unazidi kuwa mkubwa baada ya nyota huyo kutosema chochote kuhusiana na msimamo wake licha ya kuwa kocha wa Man United Jose Mourinho mwezi uliopita alisema wanasubiri maamuzi ya Zlatan.
Kituo cha TV cha Marekani kinachojihusisha na michezo FoxSports kimeandika habari kupitia ukurasa wake wa instagram wakisema Zlatan anakwenda Marekani huku picha yake inayoaminika ya kutengeneza ikionekana kavaa jezi za LA Galaxy.
Kama taarifa za Zlatan Ibrahimovic zitakuwa za kweli kuwa ataondoka Man United mwisho wa msimu akiwa kamaliza mkataba wake, itakuwa kadumu na klabu hiyo mwaka mmoja tu toka ajiunge mwanzoni mwa msimu huu akitokea Paris Saint Germain ya Ufaransa kama mchezaji huru.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |