Rais Xi Jinping wa China amewasili Palm Beach nchini Marekani, kwa mkutano wa kwanza na mwenzake wa Marekani Bw. Donald Trump, unaolenga kuelekeza uhusiano wa nchi mbili. Katika ziara hiyo ya siku mbili, Rais Xi atakutana na Bw. Donald Trump, ambapo watabadilishana maoni kuhusu uhusiano kati ya China na Marekani na masuala ya kikanda na ya kimataifa. Rais Xi pia anatarajiwa kuhudhuria tafrija ya kumkaribisha iliyoandaliwa na rais Trump wa Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |