Rais Ibrahim Boubacar Keita wa Mali amemteua Bw. Abdoulaye Idrissa Maiga kuwa waziri mkuu kuchukua nafasi ya Bw. Modibo Keita aliyejiuzulu tarehe 7.
Bw. Maiga alizaliwa mwaka 1958 huko Gao kaskazini mwa nchi hiyo. Alikuwa ameshika nafasi ya waziri wa ulinzi wa Mali kuanzia mwezi Septemba mwaka jana, pia yeye ni naibu mwenyekiti wa chama tawala cha RPM.
Hadi sasa serikali ya Mali bado haijaeleza sababu ya kujiuzulu kwa Bw. Keita, wala tarehe ya kuundwa kwa serikali mpya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |