• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri Mkuu wa China akutana na ujumbe wa wabunge wa Marekani

    (GMT+08:00) 2017-04-11 09:46:42
    Waziri mkuu wa China Bw Li Keqiang jana alikutana na ujumbe wa wabunge wa Marekani mjini Beijing, na kuwambia kuwa China inapenda kuimarisha mawasiliano na Marekani kwenye sekta na ngazi mbalimbali, ili kuwanufaisha wananchi wa pande hizo mbili.

    Bw Li amesema kuwa China na Marekani ni washirika wakubwa wa kibiashara, ambao wanaweza kunufaishana kwa njia ya kukuza ushirikiano. Amesema China inapenda kuhimiza mazungumzo ya makubaliano ya uwekezaji wa pande mbili, na kutatua masuala yaliyopo kwa njia ya mazungumzo, ili kuuhimiza uhusiano wa nchi mbili uendelee kukua kwa uwiano.

    Kwa upande wa Marekani, wajumbe wamesema Marekani inafurahia maendeleo ya China, na bunge la Marekani linapenda kuzidisha mawasiliano na China, na kuhimiza urafiki kati ya nchi hizo mbili.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako