Mfumko wa uchumi nchini Rwanda umepungua hadi asilimia 7.7 mwezi Machi kutoka 8.1 mwezi Februari kwa mujibu wa ripoti ya ya shirika la takwimu.
Afueni hiyo imetokana na kuimarika kwa bei ya vyakula,na vinywaji pamoja na umeme ,gesi na mafuta.
Benki ya kitaifa ya Rwanda aidha imeelezea hofu yake ya bidhaa muhimu kupanda tena bei kutokana na ukame na mvua chache.
Gavana wa Benki hiyo John Rwangombwa anatarajia hali hii kuendelea hivi kwa mda huu hasi wakati wa msimu wa mavuno.
Sekta ya kilimo katika nchi zote za jangwa la sahara imesababisha mfumko kutokana na ukame.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |