Okumbi alisema Paul Kiongera wa AFC Leopards anauguza jeraha, Omar Mbongi (Ulinzi Stars) amejiunga na mazoezi ya kijeshi naye Wafula ameruhusiwa kwenda nyumbani kuomboleza kifo cha mwanawe.
Kadhalika kocha huyo amewaondoa kikosini wanasoka watano wa Gor Mahia na kuwapa nafasi hizo Brian Birgen wa Ulinzi FC, Victor Majid (Chemilil FC), Zeka Wakoli (GFE FC), Victor Ogedo (Nzoia FC), Shami Mwinyi (Thika United), Ian Otieno (AFC Leopards) na James Saruni wa Ulinzi FC.
Kikosi cha Malawi kinatarajiwa kuwasili nchini Kenya Jumapili jioni kwa mechi itakayochezwa Jumanne wiki ijayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |