Wapiganaji 35 wa kundi la IS wameuawa katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa na jeshi la serikali ya Iraq katika maeneo yaliyo karibu na mji wa Mosul, kaskazini mwa nchi hiyo.
Jeshi la Iraq linaendelea na mapambano ya kuurejesha eneo la magharibi mwa mji wa Mosul, hata hivyo ukali wake umepungua kutokana na wapiganaji wa kundi la IS kuwateka nyara raia wengi katika maeneo yenye mitaa iliyobanana na njia nyembamba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |