Benki ya dunia imesema Kenya inahitaji nyumba milioni 3 ili kuzuia kuenea kwa makaazi ya mabanda.
Benki hiyo imesema kwenye ripoti yake kwamba sita kati ya kila nyumba 10 kwenye maeneo ya miji ziko kwenye maeneo ya mabanda.
Imesema miradi ya ujenzi wa nyumba itafungua nafasi za ajira, kuinua hali ya kiuchumi na kufanya sekta ya fedha kuwa imara.
Taakwimu zinaonyesha kwamba Afrika ina ukuaji wa miji wa kasi zaidi duniani huku asilimia 40 ya watu wake bilioni 1 wakiishi kwenye miji midogo na mikubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |