Ripoti ya tume ya kiuchumi ya Afrika ECA inaonyesha kwamba kanda ya Afrika Mashariki ndio ilikuwa na ukuaji mkubwa zaidi ya kiuchumi kote barani Afrika.
Tume hiyo imesema kwenye ripoti yake kwamba kanda hiyo iilikuwa na ukuaji wa asilimia 5.5 mwaka 2016.
Aidha imetabiri kwamba kutakuwa na ukuaji wa asilimia 6.0 mwaka huu ukisaidiwa na utendaji bora wan nchi za Kenya, Rwanda na Tanzania.
Nchini Kenya, uwekezaji kwenye miundo mbinu na ujenzi wa nyumba zilsaidia kukua kwa uchumu huku nayo Tanzania ikiwa na ongezeko kwenye sekta za huduma na utengenezaji bidhaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |