Wakicheza bila Mastaa wao Cristiano Ronaldo, Gareth Bale na Karim Benzema waliopumzishwa kwa ajili ya Mechi ya Marudiano ya UEFA CHAMPIONS LIGI dhidi ya Bayern Munich itakayochezwa Santiago Bernabeu Jumanne, Real walitoka nyuma kwa Bao la Duje Cop na Isco kuwasawazishia. Magoli mengine ya Madrid yamefungwa na Alvaro Morata na Isco alifunga bao la tatu na la ushindi dakika ya 90
Huko Nou Camp, mabao ya Barcelona yalifungwa na Lionel Messi bao 2, na Paco Alcacer wakati za Sociedad zilifungwa na Samuel Umtiti, aliejifunga mwenyewe, na Xabier Pieto.
Wikiendi ijayo huko Santiago Bernabeu, ni ule mtanange mkale uliobatizwa El Clasico kati ya Real Madrid na Barcelona.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |