Ofisi ya mradi wa China wa kupeleka wanaanga kwenye anga ya juu imesema, chombo cha kupeleka mizigo angani cha Tianzhou-1 kitarushwa kati ya tarehe 20 na 24 mwezi huu.
Ofisi hiyo imesema, mpaka sasa idara husika zimekamilisha maandalizi mbalimbali kwa ajili ya kurushwa kwa chombo hicho ambacho ni cha kwanza kupeleke mizigo angani kilichotafitiwa na kutengenzwa na China yenyewe. Chombo hicho kitaungana na maabara ya anga ya juu ya Tiangong-2, ili kuongeza msukumo kwake kwenye mzingo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |