Rais Xi Jinping wa China anatarajiwa kuhudhuria ufunguzi wa Jukwaa la Ukanda Mmoja na Njia Moja kwa Ushirikiano wa Kimataifa litakalofanyika tarehe 14 na 15 mwezi ujao mjini Beijing.
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi amesema, wakuu na viongozi wa nchi 28 watahudhuria mkutano huo, akiwemo rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, rais Vladmir Putin wa Russia, rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki, na waziri mkuu wa Pakistan, Nawaz Sharif.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |