Wakulima wa miwa nchini Kenya wanataka serikali ya kitaifa kuwapa pesa za kutosha kama njia moja ya kuimarisha kilimo cha miwa na uzalishaji wa sukari ambapo imepungua.
Akizungumza na wanahabari mjini Awendo, katibu mkuu wa muungano wa wakulima wa miwa nchini Bw Hezra Okoth Olodi, anasema kama serikali itawapa takriban sh bilioni 10 kwa ajili ya sekta ya miwa wataweza kupata faida kubwa ikizingatiwa kuwa baada kukata miwa hiyo watakuwa na uwezo wa kuirudisha kwa haraka.
Kiasi cha mkopo kinacho chukuliwa na wakulima wanasema hakina faida yoyote kwa wakulima.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |