Kikao hicho kimefanyika jana asubuhi huku waamuzi, wafanyakazi wa bodi ya ligi, viongozi wa simba, Kagera Sugar, waamuzi wa mechi kati ya Kagera Sugar dhidi ya African Lyon na beki Mohammed Fakhi wamehojiwa.
Awali, kamati ya Saa 72, ilikuwa imeipa Simba pointi 3 na mabao3 licha ya kufungwa kwa mabao 2-1 dhidi ya Kagera Sugar. Kamati ya Saa 72, ilibaini Kagera Sugar ilimchezesha Fakhi mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba akiwa na kadi 3za njano.
Lakini Kagera Sugar wakaendelea kusisitiza kwamba Fakhi alikuwa na kadi 2 tu za njano alizopewa katika mechi ya Mbeya City na ile dhidi ya Majimaji na si dhidi ya African Lyon.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |