Katibu mkuu wa chama cha kuogelea Tanzania (TSA), Ramadhani Namkoveka na muogeleaji mwenyewe Hilal Hilal wamesema kambi hiyo itamsaidia kufanya vyema kwenye mashindano yajayo ya kimataifa. Mashindano ambayo timu ya taifa ya kuogelea ya Tanzania, itashiriki ni ya Jumuiya ya Madola yatakayofanyika nchini Australia mwakani na yale ya Olympiki yatakayofanyika Tokyo Japan mwaka 2020.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |