Benki ya Dunia imeonya kuwa tatizo la madeni inaweza kukabiliana pigo kubwa kwa utekelezaji wa bajeti ya serikali.
Aidha inasema kuna tatizo katika utekelezaji wa bajeti ya Tanzania ambayo inapaswa kutuma ujumbe mkali kwa wa watunga sera.
Kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni ya Benki ya Dunia ni kwamba Uchumi wa Tanzania unavutwa chini na madeni ya matrilioni ya fedha.
Na madeni haya yanatishia uaminifu wa bajeti, hivyo inakuwa vigumu kuleta wadau muhimu kufadhili bajeti hiyo.
Kulingana na Benki ya Dunia mwaka jana mwezi Juni serikali ilikuwa hajalipa wauzaji na wafanyikazi karibu sh trilioni 6.5, ambayo ni sawa na asilimia 6.5 ya pato la taifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |