• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: FAO yazindua mradi wa kupunguza umaskini Rwanda

    (GMT+08:00) 2017-04-20 19:28:58

    Shirika la Umoja wa Mataifa la kilimo na chakula FAO nchini Rwanda limezindua mradi mpya unatarajiwa kupunguza viwango vya umaskini katika wilaya sita nchini humo.

    Mradi huo wa miezi 18 utatekelezwa kwa gharama ya dola milioni 286 na unalenga kuongeza mapato yatokanayo na kilimo na pia lishe kwa jamii.

    Familia maskini kutoka mikoa ya Rubavu na Nyabihu itafaidika na mradi huo.

    Wanaofaidi watapewa mbuzi au kondoo tatu, kuku, nguruwe za franc 80,000.

    Zaidi ya watu 19,000 huku franc bilioni 3 zikitumika kuwanunuliwa mifugo.

    Akiongea wakati wa uzinduzi huo mjini Kigali, katibu wa kudumu kwenye wizara ya serikali za mitaa na maswala ya jamii Odette Uwamariya, alisema baadaye miradi sawa na huo itaanzishwa kote nchini.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako