• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda: Biashara ya sakamu Uganda yapungua kutokana na mbinu duni za uvuvi

    (GMT+08:00) 2017-04-20 19:30:39

    Wizara ya kilimo na mifugo nchini Uganda imesema serikali inapoteza fedha nyingi kwenye sekta ya uvuvi kutokana na mbinu duni za kuvua samani.

    Waziri kwenye wizara hiyo Vincent Bamulangaki Ssempijja, amesema kwa sasa Uganda inapata dola milioni 150 kila mwaka lakini awali wakati viwanda vyote vilikuwa vinafanya kazi ilipata dola milioni 400.

    Alisema iwapo uratibu unaofaa ungewekwa kwenye sekta hiyo basi auzo yangefikia dola miliono 800 kwa mwaka.

    Sekta hiyo inachangia asilimia tatu ya uchumi wa kitaifa na hivyo Ssempijja anasema inafaa kulindwa.

    Amesema awali kulikuwa na viwanda 23 vya samaki lakini sasa 13 vimefungwa kutokana na uhaba wa samaki unaochangiwa na njia duni za kuvua.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako