China imerusha chombo cha kwanza cha kupeleka mizigo kwenye anga ya juu Tianzhou-1 leo jioni, ikiwa ni hatua muhimu kwa nchi hiyo katika kujenga kituo cha anga ya juu ifikapo mwaka 2022.
Chombo hicho kimerushwa kutoka kituo cha kurusha vyombo vya anga ya juu cha Wenchang, mkoani Hainan, kusini mwa China. Kitakpofika kwenye anga ya juu, chombo hicho kitatia nanga katika maabara ya Tiangong-2, kutoa mafuta na mahitaji mengine, na kufanya majaribio katika anga ya juu kabla ya kurudi duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |