Serikali ya Rwanda sasa imeanza kuwatumia wanajeshi wake kupambana na viwavi jeshi ambao wameharibu mimea hasa mahindi katika maeneo kadhaa nchini humo
Viwavi hao wamesababishia wakulima hofu ya kupata mavuno machache ikiwa hawataangamizwa.
Wanajeshi tangu jana wamekuwa wakinyunyiza dawa katika maeneo yay a wilaya ya, Kicukiro.
Msemaji wa jeshi kanali René Ngendahimana, amaesema zoezi hilo litafanyika nchini kote ili kuangamiza wadudu hao wanaotishia usalama wa chakula.
Wadudu hao wameathiri nchi kadhaa afrika mashariki na kusini zikiwemo Uganda, Kenya na Afrika Kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |