Shirika la Fedha la Kimataifa IMF limesema huenda litaongeza makadirio ya ukuaji wa uchumi wa China kwa mwaka wa 2017 kutokana na mwanzo wenye nguvu wa mwaka huu.
Naibu mkurugenzi wa IMF kanda ya Asia Pasifiki Markus Rodlauer ameliambia shirika la habari la China Xinhua kuwa katika robo ya kwanza viashiria mbalimbali vya kiuchumi nchini China vilikuwa vizuri, na pato la taifa liliongezeka kwa kiwango kikubwa kuliko ilivyokadiriwa na kufikia asilimia 6.9 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |