Askari wasiopungua 135 wameuawa na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa katika shambulizi lililofanywa na kundi la Taliban dhidi ya kambi ya jeshi la Afghanistan iliyo mkoani Balkh, kaskazini mwa nchi hiyo.
Duru zinasema washambuliaji 10 wameshiriki katika shambulizi hilo, 7 kati yao waliuawa kwa kupigwa risasi na vikosi vya usalama baada ya mapigano ya masaa manne, magaidi wawili walijilipua kwa mabomu huku mmoja akikamatwa na mkanda wa mabomu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |