Wizara ya ulinzi ya Russia imesema imerekodi matukio 14 ya kukiuka usitishaji vita nchini Syria ndani ya siku moja iliyopita. Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo inasema Uturuki imerekodi matukio 26 ya ukuikaji wa usitishaji vita, lakini bado hayajathibitishwa na upande wa Russia. Russia na Uturuki ni wadhamini wa usitishaji vita ulioanza kutekelezwa Desemba 30 mwaka jana katika maeneo yote nchini Syria.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |