• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri wa mambo ya nje ya China ataka sauti ya amani na busara kuhusu suala la peninsula ya Korea

    (GMT+08:00) 2017-04-24 09:45:31
    Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi amesema katika siku za karibuni kumekuwa na vitendo na kauli nyingi za kupinzana na za uchochezi kuhusiana na suala la peninsula ya Korea, na kusisitiza kuwa utatuzi wa suala hilo unahitaji sauti ya amani na yenye busara.

    Waziri Wang Yi amesema hayo kwenye mkutano na wanahabari baada ya kukutana na mwenzake wa Ugiriki huko Athens. Alisema China siku zote inashikilia msimamo thabiti wa kuunga mkono kuondoa silaha za nyuklia katika peninsula ya Korea na kulinda amani na utulivu kwa njia ya amani. Amesema ingawa China si kiini cha mgongano huo, imeendelea na juhudi za kurudisha mazungumzo ya amani kati ya pande husika, na hivi karibuni imetoa pendekezo la ufumbuzi linaloungwa mkono na nchi nyingi. Bw. Wang ameongeza kuwa China pia inazikaribisha nchi nyingine kutoa suluhisho lao, zikiwa na nia ya dhati ya kulitatua suala hilo kwa amani.

    Bw. Wang Yi pia amesema China itaendelea kutekeleza majukumu yake na kutoa mchango wa kiujenzi katika kutatua suala la nyuklia la peninsula ya Korea.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako