• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Mataifa walaani kutokuwepo kwa uwajibikaji wa uhalifu Sudan Kusini

    (GMT+08:00) 2017-04-24 10:36:00
    Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kutokuwepo kwa uwajibikaji wa vitendo vya uhalifu vilivyotendwa kwenye vurugu katika mji wa Wau, kaskazini magharibi mwa Sudan Kusini, ni changamoto kubwa kwa nchi hiyo.

    Kiongozi wa Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini masuala ya haki za binadamu Bw Eugene Nindorera amesema hakuna yeyote aliyekamatwa au kutiwa mbaroni kwa kuhusika na hatia ya mauaji mjini Wau.

    Vurugu zilizotokea mjini Wau mwezi Aprili zimesababisha vifo vya askari 19 wa jeshi la Sudan Kusini SPLA, na wananchi wengine wasiopungua 28. Serikali ya jimbo la Wau imeanzisha kamati kwa ajili ya kuandaa ripoti ya uchunguzi ili kuwatambua wahusika wa vurugu na kuwafikisha mbele ya sheria.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako