Taarifa iliyotolewa na jeshi la Afghanistan imesema, wapiganaji hao wameuawa katika mashambulizi ya anga na ardhini yaliyofanywa na vikosi vya usalama vya Afghanistan katika wilaya ya Achin mkoani Nangarhar katika saa 24 zilizopita.
Wakati huohuo, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Geng Shuang amesema, China inafuatilia kuongezeka kwa mgogoro wa nchini Afghanistan. Geng amesema hayo kutokana na shambulizi lililofanywa na kundi la Taliban dhidi ya kambi ya jeshi la nchi hiyo karibu na mji mkuu wa jimbo la kaskazini la Barh na kusababisha vifo vya watu 140.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |