Taarifa iliyotolewa na jeshi la Uturuki inasema operesheni hiyo inayolenga kulizuia PKK kufanya magendo ya silaha zinazotumika kufanya mashambulizi nchini Uturuki, imeharibu makazi, ghala la silaha na vituo vya mawasiliano ya kundi hilo.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Bw. Mark Toner amesema Uturuki haikuwasiliana na Marekani au nchi nyingine za muungano kabla ya kufanya mashambulizi hayo. Amesema wanasikitishwa kuwa mashambulizi hayo yamesababisha vifo kwa wapiganaji wa Peshmerga, wanaosaidia kupambana na kundi la IS.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |