Ikulu ya Marekani imeanzisha tovuti mpya kuonesha mafanikio aliyopata rais Donald Trump wa nchi hiyo katika siku zake 100 za mwanzo tangu aingie madarakani. Tovuti hiyo inasema, rais Trump amechukua hatua madhubuti kurejesha ustawi wa nchi, kuimarisha usalama wa taifa na kuongeza uaminifu wa serikali. Katika kipindi hicho cha siku 100, serikali yake imeongeza nafasi laki tano mpya za ajira na kuzuia asilimia 61 ya vitendo vya kuingia Marekani kiharamu kwa kuvuka mipaka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |