Msemaji wa serikali ya mkoa wa Jowzjan, Afghanistan amesema waasi wa tawi la Kundi la IS nchini Afghanistan wamepambana na Kundi la Taliban Jumanne mkoani Jowzjan, kaskazini mwa nchi hiyo, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 91.
Msemaji huyo amesema mapambano hayo yamesababisha vifo vya waasi 76 wa Kundi la Taliban, na wengine 56 kujeruhiwa, kwa upande wa Kundi la IS, waasi 15 wameuawa na wengine 12 kujeruhiwa.
Ameongeza kwamba mapambano hayo ya kugombea maeneo, bado hayajaisha hadi sasa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |