Baraza la seneti la Burundi limeidhinisha makubaliano yenye thamani ya dola za kimarekani milioni 50 na Benki ya dunia kwa ajili ya kusaidia sekta ya afya nchini humo. Waziri wa afya ya umma na udhibiti wa Ukimwi wa Burundi Bi. Josiane Nijimbere amewaambia maseneta kwamba fedha hizo zitasaidia programu ya miaka minne itakayoanza Julai mwaka huu, ya kutoa huduma za matibabu bila malipo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kina mama wajawazito na wanaojifungua.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |