Kamanda anayeunga mkono serikali ya Yemen kanali Abdullah al-Rashedi pamoja na askari 7 waliuawa jana kwenye shambulizi la kombora lililofanywa na wapiganaji wa Houthi katika mkoa wa Marib, kaskazini mashariki mwa Yemen. Shambulizi hilo lililolenga kituo cha jeshi la serikali kwenye wilaya ya Serwah, magharibi mwa mkoa wa Marib, pia lilijeruhi watu wengine 20, wengi wao wakiwa mahututi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |