Wizara ya ulinzi ya Russia imesema ilirekodi matukio 15 ya kukiuka usitishaji vita nchini Syria katika saa 24 zilizopita, 9 yakiwa yametokea katika jimbo la Damascus. Taarifa ya kila siku inayotolewa na wizara hiyo kwenye tovuti yake imesema, Uturuki pia imerekodi matukio 12 ya kukiuka usitishaji vita, lakini hayajathibitishwa na Russia. Russia na Uturuki ni wadhamini wa makubaliano ya kusimamisha vita kote nchini Syria yaliyoanza kutekeleza Desemba 30 mwaka jana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |