Watu watano wamefariki dunia na wengine tisa wamejeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea mkoani Nampula, kaskazini mwa Msumbiji.
Kwa mujibu wa Radio ya Msumbiji, basi moja la serikali lililokuwa likisafirisha wafanyakazi liligongwa na basi lingine linalomilikiwa na kampuni binafsi ya usafiri.
Hospitali kuu ya Nampula imesema, watu watatu walifariki papo hapo na wengine wawili walifariki wakiwa njiani kupelekwa hospitali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |