Habari zinasema kundi la Jaish al-Islam linaloungwa mkono na Saudi Arabia lilianza mashambulizi dhidi ya kundi la Nusra Front linaloungwa mkono na Qatar na kusababisha vifo vya raia wasiopungua watano.
Huku, watu takriban 3,000 waliandamana huko Ghouta Mashariki wakizitaka pande hizo mbili zisitishe mapambano, ambapo kundi la Jaish al-Islam liliwafyatulia risasi na kuwatimua.
Wachambuzi wanaona kuwa mapigano hayo yameakisi mgongano wa maslahi ya pande zinazoyaunga mkono makundi hayo, ambapo yote yanagombea udhibiti imara wa maeneo ya mashariki wa Damascus.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |