Watu wawili wameuawa na wengine saba kujeruhiwa jana jioni katika shambulizi la risasi linalohusiana na ubaguzi wa rangi katika eneo la makazi huko San Diego, Marekani.
Watu waliouawa ni pamoja na mtu anayetuhumiwa kufanya shambulizi hilo na majeruhi wengi wana hali mbaya kutokana na shambulizi hilo.
Mkuu wa Polisi wa San Diego Shelly Zimmerman amesema, mtu aliyefanya shambulizi hilo ni mwanamume wa kizungu aliyekuwa na bunduki aina ya machine gun, ambaye aliuawa kwa risasi na maaskari watatu waliofika kwenye eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |