Chama tawala cha Uturuki AKP kimetangaza kumchagua tena rais Recep Erdogan kuwa mwenyekiti wa chama hicho baada ya yeye kuacha wadhifa huo kwa miaka mitatu kwa mujibu wa katiba ya awali. Naibu mwenyekiti wa AKP Bw. Yasin Aktay amesema, sherehe itafanyika leo kumkaribisha rais Erdogan na kumpatia tena uanachama wa chama hicho, na rais Erdogan ambaye ameongoza chama hicho kwa miaka 13 mfululizo kuanzia mwaka 2001, atachaguliwa rasmi tena kuwa kiongozi wa chama hicho kwenye mkutano maalumu wa chama utakaofanyika Mei 21.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |