Watalii wawili wa Ujerumani wamefariki dunia na wengine 18 wamejeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka katika jimbo la Fars, kusini mwa Iran. Majeruhi wamekimbizwa hospitali, wawili kati yao wakiwa mahututi. Polisi wa jimbo la Fars wamesema utelezi barabarani na kasi ya basi ndio chanzo cha ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |