• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Idadi wa wasafiri wa treni wakati wa sikukuu ya Mei Mosi nchini China yaongezeka

    (GMT+08:00) 2017-05-02 19:20:50

    Safari za treni wakati wa sikukuu ya Mei Mosi nchini China imeongezeka kwa asilimia 6.7 ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huo, ikiashiria hamasa ya kusafiri kwa jamii ya China.

    Shirika la Reli la China limesema, jumla ya safari milioni 49 zilifanyika kuanzia April 28 mpaka Mei Mosi, ikiwa ni ongezeko la safari milioni 3.09 kutoka mwaka jana. Ili kukabiliana na wingi wa abiria katika kipindi hicho, Shirika hilo liliongeza safari 1,901 za treni nchi nzima.

    Sekta ya utalii nchini China ilipata faida ya dola za kimarekani bilioni 11.5 wakati wa sikukuu ya Mei Mosi, ikiwa ni ongezeko la asilimia 16.2 ikilinganishwa na mwaka jana.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako