• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yaitaka jumuiya ya kimataifa ilinde mamlaka ya kanuni ya kutoeneza silaha za nyuklia

    (GMT+08:00) 2017-05-03 20:01:22

    Balozi wa China anayeshughulikia maswala ya silaha kwenye Umoja wa Mataifa Bw. Fu Cong amesema jumuiya ya kimataifa inapaswa kulinda na kuhimiza mamlaka, ushawishi na ufanisi wa kanuni ya kutoeneza silaha za nyuklia.

    Maandalizi ya mkutano wa 10 wa majadiliano wa mwaka 2020 kuhusu kanuni ya kutoeneza silaha za nyuklia ulifanyika jana kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa huko Vienna, na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka nchi zaidi 110 zilizosaini kanuni hiyo zikiwemo China, Marekani, Russia, Uingereza na Ufaranza ambazo zina silaha nyuklia. Mkutano huo utajadili maendeleo ya utekelezaji wa kupunguza silaha za nyuklia, na kutoeneza silaha za nyuklia na kutumia nishati ya nyuklia kwa amani.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako