Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw Mrisho Gambo amesema kwamba serikali ya Kitaifa itajenga bandari ya nchi kavu mkoani humo.
Gambo amesema Bandari hiyo itasaidia pakubwa kurahisisha usafirishaji wa mizigo haswa malighafi za viwanda na bidhaa zingine, jambo litakalochangia ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Arusha. Zaidi ya ekari 500 zimetengwa kando ili kufanikisha shughuli hii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |