Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa jana lilitoa taarifa likiihimiza Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iunde mapema serikali ya umoja, na kupitisha sheria ya uchaguzi, ili kuhakikisha uchaguzi wa rais unafanyika mwezi Desemba mwaka huu kwa mujibu wa mpango uliowekwa awali.
Baraza la usalama limezitaka pande mbalimbali kuweka kipaumbele maslahi ya wananchi, na kutatua masuala kupitia sheria na mazungumzo, na pia kuepusha matumizi ya nguvu za kimabavu na vitendo vyovyote vinavyoweza kuzidisha hali ya wasiwasi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |