Balozi mteule wa Marekani nchini China aahidi "kuleta athari chanya" kwa uhusiano kati ya Marekani na China
Gavana wa jimbo la Iowa Bw. Terry Branstad aliyeteuliwa na rais Donald Trump kuwa balozi wa Marekani nchini China amesema kama uteuzi huo ukithibitishwa, atajitahidi kuleta "athari chanya" kwa uhusiano kati ya Marekani na China.
Bw. Branstad ameutaja uhusiano huo kama "wenye sura nyingi", na kusema nchi hizo mbili zinapaswa kushirikiana kwa karibu kwenye masuala ya usalama, ikiwemo kuondoa silaha za nyuklia kwenye peninsula ya Korea na usalama wa mtandao wa internet.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |