Waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergey Lavrov amesema Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi NATO inajaribu kurejesha mazungumzo na Russia, na Russia iko tayari kwa mawasiliano na jumuiya hiyo. Lakini Bw. Lavrov amesisitiza kuwa Russia itakubali kufanya mazungumzo na NATO kwenye msingi wa usawa na kuheshimiana, na pande hizo mbili zitajadili masuala zinazofuatilia kwa pamoja, na sio matatizo yanayohitaji kutatuliwa na upande wa NATO.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |