Wasichana hao waliachiwa Jumamosi baada ya serikali kuzungumza na wapiganaji wa Boko Haram. Hadi sasa wasichana 105 kati ya wasichana zaidi ya 200 waliotekwa na kundi hilo wameachiwa huru ikiwa ni pamoja na wawili walitoroka wenyewe.
Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF limekaribisha kurudi kwa wasichana hao na kutaka vyombo husika vya Nigeria kutoa msaada wa kisaikolojia kwa wasichana hao.
Waziri wa mawasiliano wa Nigeria Bw. Adebayo Shittu ameeleza kuwa anaamini kwamba wasichana wengine waliotekwa wataachiwa haraka kutokana na juhudi za serikali. Rais Buhari ameahidi kufanya kila liwezekanalo kuwaokoa wasichana hao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |