• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya yatahadharisha kuhusu mlipuko wa homa ya Dengue huko Mombasa

    (GMT+08:00) 2017-05-08 10:05:34

    Serikali ya Kenya imetoa tahadhari baada ya kulipuka kwa homa ya dengue katika mji wa Mombasa, huku watu 153 wakithibitishwa kuambukizwa homa hiyo.

    Mtendaji mkuu wa afya wa kaunti ya Mombasa Binti Omara amesema, wagonjwa 119 wametambuliwa katika hospitali binafsi kuambukizwa homa hiyo inayoambukiza kupitia mbu, na wengine 34 walithibitishwa katika hospitali za umma katika kaunti hiyo.

    Binti Omara amesema, usimamizi umeimarishwa katika maeneo yote baada ya mlipuko wa homa hiyo kuripotiwa huko Kisauni, Jomvu, Changamwe, Nyali, Mvita na Likoni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako