Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema kuwa limewarudisha wakimbizi zaidi ya elfu 62 wa Somalia kutoka kambi ya Dadaab iliyoko kaskazini magharibi mwa Kenya tangu zoezi hilo lianze mwezi Disemba mwaka 2014.
Takwimu zilizotolewa na Shirika hilo zimeonyesha kuwa, mwaka huu pekee, wakimbizi 23,058 wamerudishwa nchini Somalia. Hata hivyo usafiri wa barabara bado umesitishwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika baadhi ya maeneo nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |