Ripoti iliyotolewa na jumuiya Internet kwenye mazungumzo ya Internet na maendeleo kanda ya Afrika inasema, mwaka jana zaidi ya robo ya watu barani Afrika walipata huduma za internet. Muunganiko uliopanuka ikiwemo maendeleo ya nyaya za baharini, umewawezesha watu milioni 341 wa Afrika kutumia huduma za Internet. Mazungumzo ya kwanza ya Internet na maendeleo kanda ya Afrika yaliyoandaliwa kwa pamoja na UNESCO na wizara ya vijana na teknolojia ya habari ya Rwanda, yatajadili jinsi Afrika inavyoweza kutumia Internet kuendeleza elimu, kuhimiza uvumbuzi na kuongeza ajira.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |